Wednesday, November 09, 2011

HAFLA YA SHUKRANI ILIYOANDALIWA NA BIAFRA SPORTS CLUB YAFANA SANA

Siku ya Ijumaa tarehe 4/11/2011 kulikuwa na hafla ya kupongezana ambayo iliandalia kwa pamoja na ya Biafra Sports Club  na 90 Degrees Pub Kinondoni. Kupongezana huko kulitokana na kukamilisha mchakato wa kuandaa/kuandika katiba ya Biafra Sports Club ambapo zoezi hilo lilifanyika kwa ushirikiano na msaada mkubwa sana wa mawazo na maoni toka kwa klabu rafiki za Namanga Jogging Club pamoja na Kunduchi kwanza Jogging Club.  

Wadau wakibadilishana mawazo wakiongozwa na Ally Masharubu mwenye kaptula

wageni toka Namanga Jogging na Kunduchi Kwanza Joggin walianza kuwasili ukumbini saa 12 jioni huku wanabiafra wakiwakaribisha kwa bashasha na majadiliano ya hapa na pale katika kuboresha klabu zetu za jogging
 
wadau wa Namanga na Biafra Jogging wakibalishana mawazo kabla ya kuingia ukumbini

Richie Richie mzee wa Riddy Sound "in the house" alitoa burudani ya nguvu kwa wadau waliohudhuria hafla hiyo ambapo alicheza nyimbo mbalimbali na kukonga nyoyo za watu wote ukumbini ambapo kila mara watu walisimama kucheza na kushangili kwa nguvu.
Richie Richie akiwazungusha wadau
Wadau wakiwa na furaha tele huku wakiburudishwa na muziki wa Richie Richie

ukawadia wakati muafaka wa kutoa shukrani kwa klabu rafiki za Namanga Jogging na Kunduchi Kwanza Jogging pamoja na wadau wote waliowezesha kukamilika kwa katiba ya Biafra Sport Club ambapo kwa niaba ya viongozi na wanachama wa Biafra Sports Club Katibu wa Biafra Sports CLub alizungumza machache ya kuwashukuru na pia alikabidhi bahasha zenye andiko rasmi la shukrani kwa viongozi wa Namanga Jogging na Kunduchi kwanza Jogging Club kama inavyookana kwenye picha hapo chini.
Makatibu paleeeeee Mbusilo Joseph (Kunduchi Kwanza Jogging) Kaka Poli (Biafra Sport Club)

Viongozi wa Namanga Jogging na Kunduchi Kwanza Jogging baada ya kukabidhiwa Bahasha

Katika kumalizia hafla na itifaki kadhaa, burudani na shangwe ziliendelea mpaka majogoo kama anavyoonekana Makamu mwenyekiti wa Biafra Jogging - Mollel aka Mutu hapo chini.
Makamu Mwenyekiti wa Biafra Sports Club (mwenye suti) Abdul Mollel

No comments:

Post a Comment