Wednesday, October 19, 2011

KUNA UMUHIMU WA MATAYARISHO YA MWILI (WARM UP) KABLA YA KUANZA MAZOEZI

WANAJOGGING WAKIFANYA "WARM UP" KABLA YA KUANZA MBIO

"Warm Up" husaidia kuuweka mwili tayari kwa ajili ya mazoezi. Vilevile husaidia kuongeza kasi ya usambazaji wa damu katika viungo pamoja na misuli ya mwili pamoja na kuupa mwii joto kwa matayarisho ya mazoezi utakayofanya ambayo husaidia kulainisha viungo vyako vya mwili, hata hivyo husaidia kulainisha mishipa inayopeleka damu kwenye moyo na kusaidia kulinda misuli isipate madhara pamoja na mifupa.

pia, husaidia kuongezeka upatikanaji na usambazaji wa hewa ya oksijeni mwilini hasa kwenye misuli na mishipa ya fahamu.

No comments:

Post a Comment