Wednesday, November 28, 2012

BONANZA LA MICHEZO NA BURUDANI LAWAKUTANISHA WADAU MBALIMBALI TAR 17 NOVEMBA, 2012

Jumamosi tarehe 17 Novemba, 2012 wanamichezo kutoka katika klabu mbalimbali za jogging pamoja na wadau wengine walikutana katika Bonanza lilioandaliwa na klabu ya michezo ya Biafra. Bonanza hilo lililopambwa na Serengeti Breweries kupitia bia ya Serengeti lilihusisha michezo pamoja na Burudani mbalimbali.

Add caption


Wanamichezo walikutana makao makuu ya Biafra, 90 Degrees pub kuanzia saa 12 asubuhi. Mazoezi ya mbio za pole pole kuzunguka maeneo mbalimbali ya manispaa ya Kinondoni, kata ya Mwananyamala zilifanyika punde baada ya vilabu vyote alikwa kufika klabuni.

Wanamichezo toka Mzimuni jogging

Mara baada ya kumaliza mbio za pole pole, wanamichezo walijongea katika viwanja vya Biafra kwa michezo mbalimbali ikiwemo mechi ya soka la veterani kati ya Care Veterani na kombaini ya vilabu vya jogging.

Care Veterani
Mchezaji wa Care Veterani Said Babaa akijiandaa kupatiwa huduma ya kwanza

Ayoub Layson wa Biafra akiongoza katika mashindano ya kutembea na yai kwenye kijiko
Michezo ni furaha
 Baada ya michezo mbalimbali wanamichezo pamoja na wadau wengine walirejea klabuni ambapo burudani mbalimbali zilikuwa zikiendelea. Hatimaye ukafika wakati ambapo baadhi ya vilabu vilitoa zawadi kwa timu ya soka ya vijana ya Biafra ambapo klabu ya Seamens ya Kigamboni walitoa mpira halisi kwa timu hiyo.

Katibu Mkuu wa Seamen Club Kaka Elly akimkabidhi zawadi ya mpira Katibu Mkuu wa Biafra Yahya Poli

Katibu Mkuu wa Biafra akiuonesha mpira kwa washiriki wa Bonanza

Katibu Mkuu wa Biafra akishangilia zawadi ya mpira pamoja na Wana-Seamen

Baada ya kuguswa na zawadi ya mpira iliyotolewa na Seamen Club kwa timu ya vijana ya Biafra, Magogoni Veterani nao walichangia pesa taslimu Sh. 5000/= kwa ajili ya mfuko wa timu hiyo. 
Magogoni Vetrani wakijinadi

Kwa mbwembwe na adabu wakiwakilisha mchango kwa mweka hazina wa Biafra Bi. Asha M. W.

Baada ya matukio hayo mahususi wanamichezo waliendelea kupata burudani mbalimbali zilizoandaliwa kwenye bonanza hilo ikiwemo promosheni ya bia ya serengeti. 
Kilinge cha wana Seamen club

Kilinge cha Kunduchi Kwanza

Kilinge cha wanabiafra

Kilinge cha Namanga Sports Club

Kaka Mudi toka Temeke Jogging akiwaimbisha wanamichezo

Mwenyekiti wa Biafra Abdul Mollel (kushoto) akiwa na Mwenyekiti wa kamati ya nidhamu ya Biafra Mustafa Muro (kulia)
Ummy wa Kunduchi Jogging (aliyesimama) akifuatilia jambo na Mwenyekiti wa Kunduchi Kwanza Asia Mohamed (mwenye shati la draft)




Wednesday, October 24, 2012

PONGEZI KWA MWANABIAFRA ROSE MWAKIBUGI KWA BIRTHDAY ILIYOPENDEZA

Wanabiafra pamoja na marafiki mbalimbali walijumuika pamoja katika sherehe ya kustukiza "suprise" ya kuzaliwa kwa mwnabiafra mwenzao Mrs. Rose Mwakibugi ambayo iliandaliwa na mwanabiafra mwingine ambaye pia ni mume wa bi Rose, kaka Robert Mwakibugi.
Keki ya Birthday
Katika kufungua sherehe hiyo Robert Mwakibugi alitumia fursa kwa kumpongeza mke wake kwa kutimiza miaka kadhaa tangu kuzaliwa kwake na pia kwa upendo alionao kwake yeye mwenyewe pamoja na familia yao kwa ujumla. 
Mr.s Rose Mwakibugi - birthday girl akiwa ofisini kwake Chimbinga Unique Pub akishangaa yanayojiri                  
Wanabiafra kutoka kushoto Robert Mwakibugi, Yahya Poli, Rose Mwakibugi, na Jaqueline Barozi

Robert Mwakibugi akimlisha mkewe Rose Mwakibugi keki ya upendo

Bw. na Bi. Mwakibugi wakimlisha keki mtoto wa Habil ambaye pia ni mwanachama wa Biafra



Kwa upendeleo maalum, kwa niaba ya wanabiafra Makamu M/Kiti Bi. Jacqueline Barozi allilishwa keki na Rose mwakibugi akisaidiana na M/Kiti Abdul Mollel

Birthday girl akipongezwa
 
Mwamabiafra Henry Maseko akitoa mkono wa pongezi

Wanabiafra Henry Maseko kushoto na King A.Y. Mpore 
KWA NIABA YA WANACHAMA WOTE KLABU INATOA PONGEZI KWA BI ROSE MWAKIBUGI KWA SHEREHE YAKE YA BIRTHDAY, TUNAMTAKIA MAISHA MAREFU YENYE FURAHA, AMANI NA MAFANIKIO. KATIBU MKUU, BIAFRA SPORTS CLUB

Monday, October 22, 2012

MAZOEZI YA MBIO ZA POLE POLE JANA JUMAPILI YAWAKUTANISHA TENA WANABIAFRA

Kama ilivyo ada, Wanabiafra kila jumapili hujikusanya na kufanya mazoezi ya mbip za pole pole (jogging) kuzunguka maeneo mbalimbali ya Kinondoni. Mazoezi ya jana yaliwakutanisha zaidi ya wanachama 30 wa Biafra ambao wakubwa kwa wadogo. 
Mwenyekiti wa Kamatu ya Uchumi Ibrahim kilasa (mwenye miwani) akikimbia pamoja na watoto

Hujachelewa kujiunga na klabu yetu, karibu sana!

Monday, October 15, 2012

BIRTHDAY YA KAWE JOGGING YAFANA

Klabu ya mchezo wa mbio za pole pole ya Kawe jana tarehe 14 Oktoba, 2012 ilitimiza mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwake ambapo mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa Naibu Waziri wa Sheria na Katiba Mh. Anjela Kairuki (Mb.). 
WanaKawe Jogging

Wanamichezo kutoka vilabu mbalimbali walishiriki katika hafla hiyo ambayo ilianza kwa mazoezi ya mbio za pole pole yaliyoanzia na kuishia katika vwanja vya Tanganyika Packers na hatimaye michezo mingine ya kuvuta kamba, kukimbiza kuku na soka la vijana ambapo Biafra Youth Football Team ilitoka sare ya bila kufungana na timu ya vijana ya Kawe.

Mara baada ya michezo kumalizika wanamichezo wote walijumuika pamoja katika ukumbi wa Massae Pub ambapo ndipo yalipo makao makuu ya Kawe jogging kwa shguli nyinginezo zilizoenda sambamba na hafla hiyo.
 


Thursday, October 11, 2012

BIAFRA JOGGING YAALIKWA KUSHIRIKI SHEREHE KUTIMIZA MWAKA MMOJA TANGU KUANZISHWA KWA KAWE JOGGING



Katika kuadhimisha mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwa klabu ya Kawe Jogging, wanachama wa klabu hiyo wamealika klabu mbalimbali zinazojihusisha na uhamasisjaji wa mchezo wa mbio za pole pole mkoa wa Dar es Salaam katika kusherehekea maadhimisho hayo. Biafra Jogging, Mzimuni Jogging, Kunduchi Kwanza Jogging na klabu ni nyinginezo kwa pamoja zitafanya mazoezi ya mbio za pole pole na kisha kushiriki katika michezo mingine kama vile kuvuta kamba na  mpira wa miguu kwa wanawake na wanaume.

Wana-Kawe Jogging wakiwa katika Magofu ya Kaole mwanzoni mwaka 2012


Biafra Jogging wakiwa pamoja na Namanga Jogging mazoezini
Klabu ya michezo ya Biafra inatoa pongezi za dhati kwa Kawe Jogging na wanachama wake wote katika sherehe hizo za kutimiza mwaka mmoja. 

WE! WE! MAZOEZI NI AFYA, ACHA KUJIACHIA

Monday, October 01, 2012

FRANCIS CHEKA AMTWANGA TENA KARAMA NYILAWILA

Jumamosi iliyopita tarehe 29 Oktoba, 2012 mtoto wa Kinondoni Msisiri ambaye kwa sasa anauwakilisha vyema mkoa wa Morogoro Francis Cheka alizidi kuonesha ubabe kwa mabondia wenzake hasa wa Tanzania baada ya kumtandika kwa TKO katika raundi ya sita mwanamasumbwi mwenye makeke na maneno mengi Kalama Nyilawila. Mpambano huo uliopigwa katika ukumbi wa PTA Sabasaba ulishuhudiwa na mamia ya mashabiki wa mchezo wa ngumi huku mgeni rasmi akiwa ni Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Afande Suleiman Kova. 

Bondia Francis Cheka akipima uzito

Bondia Kalama Nyilawila akipima uzito
Mpambano huo ulikuwa ni wa kuwania ubingwa wa mabara wa UBO mkanda ambao ulikuwa wazi ulizidi kumweka katika nafasi nzuri ya mchezo wa ngumi duniani Francis Cheka ambaye ni bingwa wa ngumi za kulipwa anayetambuliwa na vyama vya ICB, IBF na WBC na sasa UBO.
Bondia Karama Nyilawila  kulia akijitahidi kukwepa makonde ya Francis Cheka

Bondia Francis Cheka (kulia) akimsukumia konde Kalama Nyilawila


Katika raundi tano za kwanza Nyilawila alionyesha kumdhibiti kiasi Cheka kwa kumchezea 'kibabebabe' huku akitumia nguvu nyingi kujihami hali iliyopelekea baadhi ya mashabiki wa Nyilawila kushangilia kwa nguvu huku wa kuwa mwisho wa tambo za Cheka ulikuwa umewadia.
Hata hivyo raundi ya sita ilipoanza Cheka alionyesha amebadilika na hasa baada ya kocha wake Abdallah Saleh 'Komando' kupanda ulingoni na kuzungumza na bondia huyo na kumshushia kipigo Nyilawila, ambapo moja ya makonde matatu ya mfululizo yalimpeleka chini mpinzani wake ambapo mwamuzi wa pambano hilo, Jerome Waluza alimhesabia Nyilawila ambaye alijitahidi kuinuka, lakini ghafla akaonyesha ishara kwamba asingeweza kuendelea na pambano hilo.  
Baada ya kuonyesha ishara hiyo, mashabiki wa Cheka walilipuka kwa shangwe kkushangilia ushindi huo wa TKO. Itakumbukwa kuwa hii ni mara ya ili kwa Cheka kumpiga Nyilawila

Mgeni rasmi Kamanda Kova (kulia) akimnyanyua mkono Francis Cheka kuashiria ushindi
Klabu ya Michezo ya Biafra inampa pongezi nyingi Bondia Francis Cheka (mtoto wa nyumbani) kwa ushindi huo. 

(Picha na habari kwa hisani ya  Super D Boxing Blog na Shaffih Dauda Blog)

Friday, September 28, 2012

KLABU YA MICHEZO YA BIAFRA YAJIPANGA KUWAKABIDHI RASMI BARUA ZA UTEUZI VIONGOZI WAKE JUMAPILI TAREHE 30 SEPTEMBA, 2012

Mwenyekiti mteule wa Klabu ya Michezo ya Biafra Bw. Abdul Mollel anawakaribisha wanachama, mashabiki pamoja na wadau wote kwa ujumla katika hafla ya kukabidhi barua za uteuzi kwa viongozi wote waliochaguliwa katika uchaguzi uliofanyika tarehe 16 Septemba, 2012. Hafla hiyo itafuatiwa na mazoezi ya pamoja ya mbio za polepole zitakazofanyika kuanzia majira ya saa 12:15 asubuhi makao makuu ya klabu 90 Degrees Pub Kinondoni na kuishia hapo hapo klabuni. 
Mwenyekiti mteule wa Biafra Abdul A. Mollel akitoa shukrani kwa wasimamizi wa uchaguzi, wanachama na wadau wote kwa kuweza kufanikisha uchaguzi huo.
Akielezea mazoezi ya mbio za pole pole (jogging) siku hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi ya Klabu Mr. Michael Silili alibainisha kwamba mazoezi yataanzia klabuni saa 12:15 asubuhi na kupitia barabara ya Kawawa na kuvuka Moroko kisha barabara ya migombani mpaka hospitali ya Mikocheni hadi viktoria na kukatisha baraba ya kuelekea mwananyamala kisha kupitia barabara ya kwakopa hadi kanisani na kumalizia klabuni kupitia barabara ya Isere.
Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi Michael Silili (Kulia) akiwa na mjumbe wa kamati hiyo Nancy Rafael wakifuatilia jambo kwa makini.

Akimalizia, Katibu Mkuu Mteule Bw. Yahya Poli aliwakaribisha wadau wote hata wale ambao si wanachama kwa mazoezi ya pamoja na baadaue hafla hiyo ya kukabidhi rasmi barua za uteuzi kwa viongozi wa klabu. Kwa wale ambao wanapenda kushiriki basi wanaweza kuwasiliana na katibu huyo kwa namba ya 0715253653.

 WE! WE! MAZOEZI NI AFYA, ACHA KUJIACHIA!

Tuesday, September 25, 2012

BIAFRA YOUTH FOOTBALL TEAM INAKUOMBA UCHANGIA VIFAA VYA MICHEZO ILI KUENDELEZA VIPAJI VYA SOKA KWA VIJANA

Timu ya vijana ya Biafra inawaomba wadau wote wa michezo uwezeshwaji wa vifaa vya michezo kwa ajili ya kuimarisha vipaji vyao na kulisaidia taifa kwa siku za usoni. Akizungumza baada ya mazoezi ya timu yao katika viwanja vya Biafra Kinondoni nahodha hiyo Hussein Tahidin (pichani chini) alisema timu yao zaidi ya kucheza mpira na kukuza vipaji vyao lakini pia wanapata fursa ya kuwa pamoja kama marafiki na kujiondoa kwenye vishawishi mbalimbali na tabia zisizofaa kwenye jamii. 
Hussein Tahiddin - Nahodha
 Wakibainisha mahitaji yao, nahodha huyo pamoja na wachezaji wenzake wameeleza kwa masikitiko kuwa wanahitaji mipira, jezi, viatu, soksi, koni za mazoezi, nyavu za magoli pamoja na vifaa vingine vya michezo kwa kadri wadau watakavyoona vinafaa kwa wachezaji hao. 




Pia kwa kupitia uongozi wa klabu yao ya Biafra Sports Club vijana hao wanaomba udhamini wa timu yao ili waweze kushiriki mashindano mbalimbali ili waweze kupima uwezo wao.

MDAU! KAMA UMEGUSWA NA MAOMBI YA VIJANA HAWA NA UNGEPENDA KUWASAIDIA, UNAWEZA KUWASILIANA NA KATIBU MKUU WA BIAFRA SPORTS CLUB KWA SIMU +255 715 253 653, BARUA PEPE: biafra.jsclub@gmail.com

MISAADA YOTE ITAKAYOTOLEWA ITATANGAZWA HAPA!

Monday, September 24, 2012

TANZIA TANZIA TANZIA TANZIA

Klabu ya Michezo ya Biafra pamoja na wadau wake wote wanaungana kwa pamoja katika msiba wa mama mdogo wa mwanachama wake Bi. Betty Mdeka ambaye ni mjumbe katika kamati ya Uchumi, Mipango na Fedha ya Klabu.Shughuli za mazishi zinafanyika nyumbani kwa marehemu maeneo ya Sinza Legho na maziko yatafanyika katika makaburi ya Kinondoni tarehe 24 Septemba, 2012.
Bi Happy Mdeka kushoto akiwa na mwanachama wa namanga jogging

Kwa pamoja tunamuomba mwenyezi mungu amtie nguvu mwanachama mwenzetu na pia mwenyezi mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi amen!

Monday, September 17, 2012

BIAFRA YAFANYA UCHAGUZI WA VIONGOZI KWA MAFANIKIO

Jumapili ya tarehe 16 Septemba 2012 ilikuwa ni siku ya uchaguzi wa viongozi wa klabu. Uchaguzi huo ulifanyika chini ya usimamizi wa viongozi wa michezo wilaya ya Kinondoni. Kufanikiwa kwa uchaguzi huo ambao ulifanyika katika makao makuu ya klabu, 90 Degrees Pub Kinondoni kulitokana na hamasa ya wanachama kujitolea katika kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kama zilivyobainishwa katika katiba ya klabu. 
BAADHI YA WANABIAFRA WAKIWA KLABUNI KWA AJILI YA UCHAGUZI MKUU SEPTEMBA 16, 2012          

Wagombea wa nafasi mbalimbali wakisubiri kuanza kwa zoezi la uchaguzi kutoka kushoto ni Ibrahim Kilasa, Freddy Mwesigwa (wagombea nafasi ya Kamati ya Uchumi na Mipango), na Abdul Mollel (mgombea nafasi ya Mwenyekiti)



Bi. Jacqueline Barozi (mgombea nafasi ya Makamu M/Kiti) akiwa na Mustafa Muro (mgombea Kamati ya Nidhamu na Rufaa




Nancy Raphael (mgombea kamati ya Ufundi) katikati akiwa na wagombea wenza Mossi Saidi (kushoto) na Boniface Banga (kulia)
 UCHAGUZI huo pia ulihudhuriwa na klabu rafiki za Namanga na Kunduchi kwanza ambapo wanachama toka klabu hizo walijumuika kwa pamoja na Wanabiafra katika kuhakikisha zoezi hilo la uchaguzi linafanikiwa. Wakiongozwa na Mwenyekiti wao Bi. Asia Mohamed, Wanakunduchi Kwanza waliwasili katika makao maku ya klabu ya Biafra majira ya saa nne asubuhi na muda mfupi baadae wanachama wa Namanga Sports Club nao waliwasili eneo hilo.
Mwenyekiti wa Kunchi Kwanza Jogging (wa kwanza kushoto) akiteta jambo na baadhi ya Wanakunduchi Kwanza


John Gako kutoka Namanga akiomba utaratibu toka kwa 'floor manager' wa shughuli Bi. Magreth Warisanga (aliyesimama)
VIONGOZI kutoka idara ya Michezo Manispaa ya Kinondoni waliwasili ukumbini hapo majira ya saa sita mchana na mara baada ya kupokelewa na kutoa salam zao za uchaguzi, moja kwa moja walitoa mwongozo wa namna zoezi zima la uchaguzi litakavyofanyika baada ya kuridhika na maandalizi ya uchaguzi wenyewe. 
Mr. Mrimi kutoka idara ya Michezo Manispaa ya Kinondoni (Katikati) akiteta jambo na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Balozi Msolomi, Isere, Mwinyimadi Tambaza (kushoto) msimamizi wa soka kwa watoto wadogo KIDYOSA

Wasimamizi wa uchaguzi wakifuatalia kwa makini maelezo ya mgombea (haonekani pichani)
MARA baada ya kukamilika kwa zoezi la kujieleza, wanachama walianza moja kwa moja zoezi la upigaji kura ambapo baada ya kukamilika kwa zoezi hilo wagombea wa nafasi za juu za klabu walipendekeza mawakala wao katika zoezi la kuhesabu kura.
Mawakala wa wagombea pamoja na wasimamizi wa uchaguzi wakiwa katika zoezi la kuhesabu kura

Zoezi la kuhesabu kura likiendelea

zoezi la kuhesabu kura likiendelea

Wagombea wa nafasi ya Mwenyekiti na Makamu wake pamoja na wagombea wengine wakisubiri kwa hamu matokeo ya uchaguzi

Wagombea wa nafasi ya Kamati ya Ufundi wakisikiliza matokeo ya uchaguzi kwa hamu
ZOEZI la kuhesabu kura ambalo lilidumu kwa takriban masaa mawili lilikamilika na hatimaye msimamizi mkuu wa uchaguzi pamoja na jopo lake walirejea katika ukumbi wa mkutano na moja kwa moja kuanza kutangaza matokeo ya uchaguzi kwa kuanzia na wateule wa kamati za Ufundi, Uchumi na Mipango, Nidhamu na Rufaa na kisha Kamati ya utendaji, Mweka Hazina, Katibu Msaidizi, Katibu Mkuu, Makamau Mwenyekiti pamoja na Mwenyekiti. 
WASHINDI - KAMATI YA UCHUMI NA MIPANGO

AKIPONGEZWA KWA USHINDI WA NAFASI YA MWENYEKITI NDUGU ABDUL MOLLEL (KATIKATI)

WASHINDI WA NAFASI MBALIMBALI WAKIONGOZWA NA VIONGOZI WAKUU

MWENYEKITI MTEULE WA BIAFRA SPORTS CLUB, ABDUL MOLLEL AKITOA SHUKRANI KWA NIABA YA VIONGOZI WATEULE KWA WANACHAMA, WADAU NA MASHABIKI KWA KUFANIKISHA ZOEZI LA UCHAGUZI

MAKAMU MWENYEKITI MTEULE AKITETA JAMBO NA KATIBU MKUU MTEULE

MWINYIMADI TAMBAZA AKSISITIZA UMUHIMU WA KUIENZI TIMU YA WATOTO WA BIFRA KIDS

SHUGHULI ya uchaguzi ilikamilika majira ya saa moja jioni ambapo washindi pamoja na wanachama na wadau wengine wote walijumuika kwa burudani mbalimbali zilizotolewa ili kukamilisha siku hiyo maalum.

TUNAWAPONGEZA SANA VIONGOZI WOTE WALIOSHINDA PAMOJA NA WANACHAMA WOTE WA BIAFRA SPORTS CLUB, USHINDI WENU UWE CHACHU YA KULETA MAENDELEO YA KLABU NA MICHEZO KWA UJUMLA!