Tuesday, March 05, 2013

REQUEST FOR THE SPONSORSHIP OF BIAFRA YOUTH (U17) CUP 2013


Biafra Sports Club is organizing Biafra Cup (U17) Football competition which is scheduled to take place from the 2nd day of June to the 7th day of July. The tournament is expected to be strong and competitive one whereby 16 youth teams from various sports academies will participate in the tournament. 

Speaking about the tournament, the Secretary General of Club one Mr. yahya Poli informed that, The theme for the said competition is “IBUA NA ENDELEZA KIPAJI CHA KIJANA”. The 2013 Biafra Cup (U17) objectives are: -  
1. To provide young players and match officials with an opportunity to showcase their talent as well as  promote their physical and mental health and wellbeing, 
2. To assist young players to acquire and develop different football characteristics through contact with their peer,  
3. To mobilize young players and instill a sense of fair play in the best traditions of true sportsmanship,To raise awareness on the harmful social and cultural practices that are affecting children and youths at large such as drug abuse, HIV/AIDS and STDs, children’s rights through peer to peer discussion, distribution of leaflets and brochures, banners, e.t.c.
4. To promote and encourage other stakeholders to organize healthy, competitive recreation tournaments for young players. 
The tournament will take place during the month which the African continent and the world at large commemorate THE DAY OF AFRICAN CHILD on 16th June, 2013. The the for Day of African Child 2013 is "Eliminating Harmful Social and Cultural Practices Affecting the Children" therefore the organizing committee will use the tournament to raise awareness of children rights to commemorate  the said day.
 
The match officials from Twalipo Youth Soccer Foundation are expected to participate in the said tournament as referees and assistant referees in all 56 matches to be played. The said foundation train and provide refereeing skills to youths who are talented and interested to become referees in their future. These young referees have performed well in various youth tournaments such as Copa Coca Cola finals, Uhai Cup, NSSF Cup, e.t.c. to which they were participating as match officials.


He said further that, there will be various prizes to be awarded to the winners and other officials in different categories such as; the champion of the tournament, second winner, top scorer, the best disciplined player of the competition, best disciplined team of the competition, the best official, certificate of participation for each participating team and officials, e.t.c.

In order to meet the tournament’s outlined objective and budget successfully, facilitation as well as sponsorship is highly needed. Sponsors will play a very important role of facilitating the tournament by providing fund/grant and or facilities required for the tournament.

By sponsoring/facilitating the tournament sponsors on their part will have the opportunity to display and publicize their services or products during the matches and the tournament will be a platform whereby these sponsors will meet their customers/clients/communities especially youths, 


IBUA NA ENDELEZA KIPAJI CHA KIJANA 

CONTACT:
THE SECRETARY GENERAL,
BIAFRA SPORTS CLUB,
+255 715 253 6563
EMAIL: biafra.jsclub@gmail.com



Sunday, March 03, 2013

MAZOEZI YA MBIO ZA POLE POLE JUMAPILI TAR 3 MACHI YANOGA

Kama ilivyo ada, baada ya kuhairishwa ka safari ya kwenda kunduchi wanamichezo toka vilabu vya Namanga na Biafra waliamua kufanya mazoezi pamoja kwa kuanzia Namanga na na kuishia Biafra. Mbio hizo zilipita katika bara ya Ubalozi (USA), Old bagamoyo, Migombani, Mission Mikocheni, Mwai Kibaki, Mwinjuma, Hospitali ya Mwananyamala, Dunga, Kawawa na kuishia 90 Degrees Pub ambapo ni Makao makuu ya klabu y Biafra. 
Jogging barabara ya ubalozi (USA)


Katibu Mkuu wa Biafra akiongoza jahazi







Mara baada ya kumaliza jogging wanamichezo waliendelea na mazoezi ya aerobics yaliyokuwa yakiongozwa na mwanabiafra Khamis Suleiman (mwenye fulana nyekundu pichani chini).
 


Wanamichezo wote baada ya kutula walikaribishwa na Katibu Mkuu wa Biafra na baada ya pongezi za kushiriki na kumaliza mbio kwa wanamichezo wotw, taarifa mbalimbali zilitolewa ikiwemo ya  maendeleo ya mchakato wa kuanzisha Shirikisho la Jogging Manispaa ya Kinondoni pamoja na hatua zilizochukuliwa katika kuhuisha Chama cha Mchezo wa Jogging Kinondoni.
Katibu wa Biafra akiwakaribisha wanamichezo





Kutoka kushoto; Mary, Kaka Poli, na Bebee

 Safari yetu ya Kunduchi itafanyika jumapili ya tarehe 10 Machi, 2013. Karibuni wadau wote!!!

MAZOEZI NI AFYA ACHA KUJIACHIA!!!

Thursday, February 28, 2013

JOGGING YAVIKUTANISHA TENA VILABU KUNDUCHI JUMAPILI TAREHE 3 MACHI, 2013

Katika kuhamasisha mchezo wa mbio za pole pole (jogging) maeneo ya Kunduchi na kuimarisha uhusuiano wa vilabu vya jogging, Jumapili ya tarehe 3 Machi, 2013 wanamichezo kutoka katika vilabu vya Namanga, Kawe, Biafra na Kunduchi Kwanza pamoja na wadau wengine wa michezo watajumuika na kufanya mazoezi ya pamoja ya jogging ambayo yataratibiwa na klabu ya Kunduchi Kwanza ambao ndio wenyeji na waratibu wa mazoezi hayo. 
Jogging
 

Jogging ikiendelea

Baada ya mazoezi hayo, wanamichezo wote waliohudhuria watajumuika pamoja makao makuu ya klabuya Kunduchi yaliyopo Malanja Pub ambapo kutafanyika na kikao cha pamoja cha viongozi vilabu shiriki juu ya mustakbali wa mchezo wa mbio za pole pole wilaya ya Kinondoni ikifuatiwa na burudani mbalimbali.

Wadau wote mnakaribishwa!


Monday, February 25, 2013

VIONGOZI WA VILABU VYA JOGGING KINONDONI WAKUTANA NA MSAJILI WA VYAMA NA VILABU VYA MICHEZO WILAYA YA KINONDONI

Jioni ya tarehe 25 Februari, 2013, viongozi kutoka katika vilabu vya michezo vinavyojihusisha na mchezo wa mbio za pole pole walikutana na Msajili wa Vyama na Vilabu vya Michezo wilaya ya Kinondoni ndugu Jumanne Mrimi (pichani) ofisini kwake jijini Dar es Salaam. 
Ndugu Jumanne Mrimi - Msajili wa Vyama na Vilabu vya Michezo wilaya ya Kinondoni
 Viongozi waliomtembelea ni kutoka katika vilabu vya Namanga (David Mwaka na Andrew Mangole), Kawe (Mohammed Risasi, Alhaj Seif Mukhere na Khadija Mabrouk) Biafra ( Abdul Mollel na Yahya Poli) na Kunduchi Kwanza (Alphonsina Joseph).

David Mwaka (mwenye shati jekundu) - Mwenyekiti Namanga Sports Club


Alhaj Seif Mukhere  - Kaimu Katibu Mkuu Kawe Sports & Social Club

Mohammed Risasi - Mwenyekiti Kawe Sports & Social Club

Andrew Mangole - Katibu Mkuu Namanga Sports Club na Bi. Khadija Mabrouk - Makamu Mwenyekiti Kawe Sports and Social Club
Lengo la kumtembelea msajili ofisini kwake lilikuwa ni katika harakati za kufufua uhai na hamasa ya mchezo wa mbio za pole pole katika manispaa ya Kinondoni ambapo viongozi wa klabu hizo wamedhamiria kuhuisha Chama cha Mchezo wa Jogging wilaya ya Kinondoni kilichoasisiwa na aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Kinondoni wakati huo Kanali Fabian Massawe na kisha baadaye kuunda shirikisho la mchezo huo.

Yahya Poli - Katibu Mkuu Biafra Sports Club na Alphonsina Joseph - Katibu Mkuu Kunduchi Kwanza Jogging and Sports Club

Maazimio ya kikao hicho yalikuwa ni pamoja na kuwasiliana na vilabu vyote vinavyojihusisha na jogging wilaya ya Kinondoni na kuunda umoja na uongozi wa chama cha jogging.
Afisa Ushirika Manispaa ya Kinondoni (mwenye shati jeusi) akisalimiana na viongozi
Mwishoni kabisa katika majumuisho yake, msajili aliahidi kushirikiana na uongozi utakaoundwa na kutoa mwongozo wa namna ya kuunda chama hicho wakati wowote atakapohitajika kufanya hivyo, vile vile aliwaasa viongozi waliomtembelea kusambaza taarifa kwa vilabu vingine ili navyo viweze kushiriki kikamilifu.
Baadhi ya viongozi wa vilabu vya jogging katika picha ya pamoja - kutoka kushoto Jumanne Mrimi (Msajili), Abdul Mollel, David Mwaka, Mohamed Risasi, Andrew Mangole, Khadija Mabrouk, Alhaj Seif Mukhere
 

Wednesday, February 20, 2013

BIAFRA SPORTS CLUB YAPATA USAJILI RASMI

Leo tarehe 20 Februari, 2013 klabu ya michezo ya Biafra imepata usajili rasmi toka Baraza la Michezo Tanzania (BMT). Usajili huo umetokana na kutimiza masharti na kanuni zote ziliyowekwa na baraza hilo katika usajili wa vilabu vya michezo nchini Tanzania. 
Cheti cha Usajili wa Biafra Sports Club
Akizungumza wakati akikabidhi cheti hicho kwa Katibu Mkuu wa Biafra ndugu Yahya Poli, Msajili wa Vyama na Vilabu vya Michezo Tanzania Mama Rwezaula aliwapongeza wanachama wote kwa kuanzisha klabu hiyo na pia aliwasihi viongozi na wanachama kuhakikisha wanasimamia na kuilinda katiba ya klabu hiyo na kujiepusha na migogoro ili kuendeleza michezo nchini.
Barua ya Usajili wa Biafra Sports Club

 Mwenyekiti wa klabu hiyo ndugu Abdul Mollel akizungumza tokea safarini Songea, aliwapongeza wanachama wote kwa kujitolea kwao katika kuiendeleza klabu na uvumilivu pale palipotokea na vikwazo vya hapa na pale. 

HONGERA WANABIAFRA WOTE - SASA TUJENGE KLABU YETU KWA KUINUA NA KUHAMASISHA MICHEZO, UPENDO, UMOJA NA USHIRIKIANO!!!!

Monday, February 11, 2013

MATUKIO YA WANABIAFRA KATIKA WIKINDI ILIYOPITA

Wanamichezo takriban wote wana msemo wao kuwa "michezo ni afya, michezo ni furaha, michezo huwaunganisha watu". Basi hivyo ndivyo ilivyokuwa juma lililopita kwa Wanabiafra. Siku ya ijumaa tarehe 8 Februari, 2013 ambapo Wanabiafra pamoja na marafiki kadhaa walikutana na kuianza wikiendi kwa burudani ya muziki, vinywaji na nyama choma pale Chiminga Unique Pub. 
Ally Masharubu na Ayub Layson wakitafuna nyama ya mbuzi

Mwenyekiti wa Biafra Abdul Mollel alisimama kuwasalimia wanabiafra na marafiki

Kutoka kushoto; Ally Masharubu, Ayub Layson na Editha Tungaraza

Mwanabiafra Dustan Barozi (kulia) pamoja na marafiki zake

Editha Tungaraza akifaidi msosi

Makamu Mwenyekiti wa Biafra Jacqueline Barozi (aliyesimama) akichukua oda ya vinywaji


Rose Mwakibugi Almaarufu mama Chimbinga alihakikisha vinywaji vipo na vya kutosha

Robert Mwakibugi akiiwakilisha vyema Chimbinga Unique Pub
Kama unapenda kushiriki kwenye mijumuiko ya aina hii, usisite, wasiliana na Katibu Mkuu, Biafra Sports Club kwa barua pepe; biafra.jsclub@gmail.com

Friday, February 01, 2013

WANABIAFRA KUTEMBELEA VITUO VYA WATOTO YATIMA MWAKA 2013

Heri ya mwaka mpya wanachama, wapenzi, mashabiki na wadau wote wa Biafra. Januari ndio hivyo imekwisha nasi klabuni tumeanza kutekeleza mpango kazi wa mwaka 2013. Kwa mwaka huu klabu imepanga kufanya matukio makubwa manne

Viongozi wa juu wa klabu wakiwa katika kikao cha kujadili Mpango Kazi wa mwaka 2013

Kutembelea na kutoa misaada ya kibinadamu katika vituo vya watoto wanaoishi katika mazingira magumu Manispaa ya Kinondoni katika kuadhimisha siku ya Mtoto wa Afrika ambapo vituo vilivyopendekezwa vitatembelewa kuanzia tarehe 2, 9 na 16 Juni ambayo ndio kilele cha siku ya mtoto wa Afrika.
Binti kutoka kituo cha Hanasif akiwa na zawadi mwaka 2011
 Mwezi Juni na Julai pia klabu itaendesha mashindano ya Soka kwa timu za vijana wenye umri chini ya miaka 17 itakayojulikana kama Biafra Cup U17. Kombe hilo linatarajiwa kufanyika kila mwaka na litatumika katika kukuza vipaji vya mchezo wa soka kwa vijana na pia klabu itatumia kombe hilo katika kusaka wachezaji nyota na kuwasajili kwenye timu. Katika kuhakikisha wanafanya vyema kwenye michuano hiyo, timu ya soka ya vijana (U17) ya Biafra ipo katika mazoezi ya kina chini ya kiongozi wao William Masika
Kikosi cha #BYFTU17 wakiwa wamevaa jezi mpya zilizonunuliwa kwa ufadhili mchezaji mwenzao aliyehamia Norway - Hamada aka Elnino

Matukio Mengine ni Biafra Day iliyopangwa kufanyika tarehe 7 Julai, 2013, kushiriki kikamilifu katika maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani tarehe 1 Disemba, 2013 pamoja na kuhamasisha utalii wa ndani na wa michezo kwa kutembelea katika mbuga ya wanayama ya mikumi pamoja na kufanya mazoezi ya mbio za pole pole na wakaazi wa vitongoji vya Mikumi mkoani Morogoro mwanzoni mwa mwezi Disemba.

Karibu sana mdau katika kufanikisha mpango kazi huu. 

Michezo ni Afya, Michezo ni Furaha!!!! 

KWA MASWALI/MAONI/USHAURI WASILIANA NA: - 
KATIBU MKUU,
BIAFRA SPORTS CLUB
+255 715 253 653 
biafra.jsclub@gmail.com
www.facebook.com/biafrasportsclub
ISELE STREET, BALOZI MSOLOMI,
KINONDONI 
DAR ES SALAAM.  

Monday, December 24, 2012

SALAAM ZA KRISMASI NA MWAKA MPYA TOKA BIAFRA!

Wakati wakristo wakiwa katika maandalizi ya sikukuu ya kuzaliwa mwokozi, Yesu kristo mnamo tarehe 25 Disemba pamoja na maandalizi ya kuuaga mwaka 2012 na kuukaribisha mwaka 2013, klabu ya michezo ya Biafra inapenda kuwatakia wanachama, wapenzi, mashabiki pamoja na wadau wote wa michezo krismasi njema pamoja na heri ya mwaka mpya 2013.

Katika kipindi hiki cha mapumziko ya sikukuu, mazoezi yataendelea kila jumapili kama kawaida! Karibuni wote.

Wednesday, December 05, 2012

HABARI MCHANGANYIKO ZINAZOHUSU VILABU MBALIMBALI VYA JOGGING MKOA DAR ES SALAAM

Mwezi disemba ndio umeingia. Katika mfumo wa kupeana taarifa mbalimbali zinazohusu klabu zetu zinazojihusisha na mchezo wa mbio za pole pole (jogging), katika wiki ya kwanza na ya pili ya mwezi disemba kuna matukio kadhaa yaliloyofanyika na yatakayofanyika. Kama ilivyo ada, klabu ya michezo ya Biafra ilijumuika pamoja na klabu ya Namanga katika na kufanya mazoezi ya pamoja jumapili ya tarehe 2 Disemba. 

Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Ally Selemeani (mwenye bukta nyeusi) akiiwakilisha vyema Biafra
Mazoezi hayo yaliyofanyika kuzunguka barabara na mitaa mbali ya Namanga na Msasani yalianzia na kumalizikia Leecars Pub ambapo ni makao makuu ya klabu ya Namanga. Mara baada ya mazoezi ya pamoja, wanamichezo wote walijumuika na kujadiliana machache kwa ajili ya maendeleo ya klabu zote ikiwemo pea kupashana taarifa mbalimbali.

Kule Magomeni nako, klabu za Mzimuni na Taifa Jogging zilikutana na kufanya mazoezi ya pamoja ya mbio za pole pole na kisha kucheza mechi za mpira wa miguu (wanaume) na mpira wa pete (wanawake). Picha zote za michezo kati ya Taifa na mzimuni Jogging ni kwa hisani ya Taifa Jogging.
Wana Taifa na Mzimuni Jogging kwenye mchakamchaka

Kipindi cha mapumziko kwa mechi ya mpira wa miguu wanaume

Wachezaji wa mpira wa pete kutoka Taifa Jogger katika picha ya pamoja

Klabu ya michezo ya Namanga imejiandaa kufanya mkutano mkuu wa mwaka wa wanachama wake mnamo tarehe 9 Disemba, 2012. Akitoa taarifa ya kufanyika kwa mkutano huo mbele ya makatibu wa vilabu vya Biafra, Msasani na Kunduchi Kwanza, Katibu Mkuu wa Namanga ndugu Mangole alieleza kuwa mkutano huo unatarajiwa kufanyika katika ukumbi wa Ndege Beach nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam. Maandalizi ya mkutano huo yanaendelea. Alieleza kuwa vilabu rafiki vyote vitaalikwa kuhudhuria mkutano. 
Mwenyekiti wa namanga Sports Club ndugu David Mwaka (aliyesimama) akichangia mada kwenye kikao cha maandalizi ya mkutano mkuu: Picha kwa hisani ya John Badi)
 Kwa habari zaidi kuhusu mkutano huo bofya hapa.

TUNAWATAKIA WANA NAMANGA MKUTANO MKUU WENYE MAFANIKIO

Saturday, December 01, 2012

1.12. 2012: SIKU YA UKIMWI DUNIANI

Tangu Disemba 1, 1988 dunia imekuwa ikiadhimisha siku ya UKIMWI duniani. Wazo la kuadhimisha siku hiyo lilitolewa na James W. Bunn naThomas Netter ambao walikuwa ni maofisa habari (Global Programme on AIDS) kwenye Shirika la Afya Duniani. Dhumuni la kuadhimisha siku hiyo ni kutoa fursa kwa watu duniani kote kuungana katika mapambano dhidi ya VVU
Utepe Mwekundu
Huu ni wakati muafaka kwa jamii nzima wakiwemo wanamichezo pia kutafakari juu ya janga la UKIMWI. 

UKIMWI UNAUA! CHUKUA HATUA SASA, JILINDE NA MLINDE MWENZAKO PIA.