Tuesday, June 19, 2012

Monday, June 18, 2012

BIAFRA KIDS YAIZAMISHA TEMEKE KIDS KWA MABAO 3 - 0

Katika kujiweka fiti kwa ajili ya kushiriki michuano ya Winome mwezi Julai mwaka 2012, timu ya Biafra Kids ilichuana na Temeke Kids katika uwanja wa Zakheem Mbagala. Mechi hiyo iliyochezwa majira ya saa sita mchana ilishuhudiwa na watazamaji zaidi ya mia tano ambao ni wanamichezo kutoka katika vilabu mbalimbali vya michezo mkoani Dar es Salaam.

Kikosi kazi cha Biafra Kids




Mchezaji wa Soka Aziza (Biafra Ladies) mwenye suruali nyeusi akifuatilia mechi kwa makini


Biafra Kids wakitoka uwanjani kwa mapumziko

Pamoja na uwanja kuwa na michanga mingi, vijana walionyesha kandanda safi kiasi cha kushangiliwa muda wote na hadi mpira unakwisha Biafra Kids walikuwa washindi wa mechi hiyo kwa mabao 3 - 0.



VILABU KADHA VYA 'JOGGING' MKOA WA DAR ES SALAAM VYAKUTANA NA KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA NA TEMEKE JOGGING

Jumapili ya tarehe 17 Juni, 2012 ilikuwa ni siku njema kwa wanamichezo katika mkoa wa Dar es Salaam. Vilabu zaidi ya 15 vya michezo, hasa vinavyohamasisha mchezo wa mbio za pole pole "jogging" vilifanya mazoezi ya pamoja kwa mwaliko wa klabu kongwe ya Temeke. Wanamichezo zaidi ya mia sita walikusanyika katika uwanja wa Taifa na saa 12:30 asubuhi walianza safari ya kuelekea Mbagala katika ukumbi wa Dar-Live kisha katika viwanja vya Zakheem kwa mchezo wa mpira wa miguu.
Biafra Jogger wakiongoza msafara wa wana-jogger


Biafra Kids wakiongoza Biafra Jogger








Baadhi ya wanakunduchi Kwanza





Makamu Mwenyekiti wa Biafra Ms. Jacqueline Barozi akiingia Darlive



Mwenyekiti wa Biafra (mwenye bukta ya bluu) akishiriki aerobics



Wanabiafra walioshiriki mazoezi katika picha ya pamoja ndani ya Darlive Mbagala


Monday, June 11, 2012

Songs makes jogging fun!!

Joggers

BIAFRA JOGGING NDANI YA JEZI MPYA YAFANYA MAZOEZI YA PAMOJA NA NAMANGA NA KUNDUCHI KWANZA

Klabu ya michezo ya Biafra imezindua awamu ya kwanza ya uzinduzi wa jezi za mazoezi ya mbio za pole pole (jogging) kwa kufanya mazoezi ya pamoja na klabu za Namanga Jogging na Kunduchi Kwanza Jogging.
Wadada wa Biafra Jogging waking'aa ndani ya 'uzi' mpya



Jezi mpya ya Biafra Jogging inavyoonekana kwa nyuma

Wanamichezo wakikatiza maeneo ya polisi Oysterbay

Mazoezi hayo yaliyofanyika jana jumapili tarehe 10 Juni, 2011 yalianzia na kuishia katika klabu ya Namanga na wanamichezo walikimbia zaidi ya kilomita 8 kwa kupitia barabara za old Bagamoyo na Ali Hassan Mwinyi (Namanga, Oysterbay Polisi, Drive -Inn, Moroko, Viktoria, Sayansi, Rose Garden, Kwa Nyerere, Chama, Drive-Inn, Oysterbay Polisi na Namanga).







Wadada wa Kunduchi Kwanza waking'aa pia na uzi wao


Viongozi wa klabu zote 3 walikutana




MATUKIO KATIKA MECHI YA BIFRA KIDS DHIDI YA KOMBAINI YA KINONDONI

Katika kujiimarisha zaidi na kuongeza uzoefu wa mechi ngumu, timu ya Biafra Kids ilipokea na kukubali mwaliko wa kucheza na timu ya kombaini ya mkoa wa Kinondoni ambao wameteuliwa kutoka katika timu mbalimbali zilizoshiriki michuano ya Copa Coca Cola kwa vijana walio chini ya umri wa miaka 17 kanda ya Kinondoni. Mechi hiyo iliyochezwa katika viwanja vya Tanganyiksa Packers Kawe, siku ya J'mosi tare 9 Juni, 2012 illisha kwa Biafra Kids kupoteza mchezo huo baada ya kufungwa mabao 2 - 1.
KIKOSI CHA BIAFRA KIDS

KOMBAINI YA KINONDONI






Kocha wa Biafra Kids William Masika (kushoto) akiwa na viongozi wa Kombaini


Tuesday, June 05, 2012

BIAFRA KIDS PLAYER OF THE WEEK 4 - 10 JUNE, 2012

From this week on, we'll be presenting you the club's player of the week. The said players is chosen by the players themselves, trainers and team captains. in order for the player to be selected a player of the week, he must demonstrate highest state of discipline on and off the field, follow and keep the instructions given by the trainers, demonstrate the ability and agility of playing footbal, e.t.c.
Players and leaders of Biafra Kids 

And, the player for this week (4th - 10th June, 2012) is Ahmed Suleiman (pictured below). He joined the club in 2011. Ahmed is 16 years old studying at Hanasif Secondary School Form II. He is mong the players club enrolled in Copa Coca Cola under 17 tournament for Kinondoni Zone. His teammates calls him Mafisango because his kind of play resembles the late player who played for Simba 2011/12 season.
 


KLABU YA BIAFRA YAITISHA MKUTANO MKUBWA WA WANACHAMA, MASHABIKI NA WADAU WAKE

Katika harakati za kuiimarisha klabu, Mwenyekiti wa klabu ya Michezo ya Biafra Bw. Abdul Mollel, kupitia Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo ameitisha mkutano mkubwa ambao utawakutanisha wanachama wote, mashabiki na wadau wa klabu hiyo pamoja na wanamichezo kwa ujumla mnamo tarehe 8 Juni, 2012 siku ya ijumaa. Mkuktano huo unatarajiwa kuanza saa 12:30 jioni na kumalizika saa 2:30 usiku na utafanyika makao makuu ya klabu 90 Degrees Pub Kinondoni.
Mwenyekiti wa Biafra Abdul Mollel (kushoto) akiwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu Ally Selemani almaarufu Masharubu

Wanabiafra wakiwa klabuni

Wanabiafra: kutoka kushoto; Robert Mwakibugi, Dastan Barozi, na mgeni wao klabuni


Akitoa taarifa za mkutano huo, Katibu Mkuu wa klabu ya Biafra alieleza kuwa pamoja na masuala mengine, ajenda za mkutano huo ni: -
  1. Kupata taarifa na kujadili maendeleo ya klabu
  2.  
  3.  Ushiriki wa wanabiafra katika shughuli mbalimbali za klabu vikiwemo vikao na mazoezi,
  4.  
  5.  Kupokea mpango kazi wa mwaka wa klabu (Juni - Disemba, 2012)
  6.  
  7. Kugawa sare (uniform) kwa wanachama waliolipia.

Akitoa msisitizo, Katibu Msaidizi wa klabu Betwely Kyando (pichani chini) alieleza kuwa kikao hicho ni muhimu sana hivyo kila mwanachama, mshabiki na mdau wa Biafra anapaswa kuhudhuria bila kukosa kwa kuwa masuala yatakayojadiliwa yatasaidia harakati za kuimarisha klabu na mchakato wa kuleta maendeleo kwa wanachama kwa ujumla.
Betwely Kyando - Katibu Msaidizi, Biafra Sports Club

Kwa maelezo, maoni, ushauri, au ungependa kushiriki kwenye mkutano huo, wasiliana na Katibu Mkuu kwa barua pepe (biafra.jsclub@gmail.com) au kwa simu +255 715 253 653.



NYOTE MNAKARIBISHWA